Header Ads

Baada ya kauli ya Rais Magufuli, IGP Sirro afanya mabadiliko haya



Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini(IGP), Simon Sirro amefanya mabadiliko ya Makamanda wa Polisi kwa baadhi ya mikoa

Katika mabadiliko hayo, Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Deusdedit Nsimeki aliyekuwa Makao Makuu ya upelelezi Dar anakwenda kuwa RPC wa Simiyu

RPC wa Morogoro, Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Ulrich Matei anakwenda kuwa RPC wa Mbeya na Kaimu RPC wa Mbeya Kamishna Msaidizi, Mussa Taibu amehamishiwa Makao Makuu Dar

Aidha, RPC wa Tabora Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Wilbroad Mutafungwa anakuwa RPC wa Morogoro, nafasi yake ikichukuliwa na Kamishna Msaidizi, Emmanuel Nley kutoka Makao Makuu Dar

Katika Mabadiliko mengine, Ofisa Mnadhimu wa Geita Kamishna Msaidizi, Stanley Kulyamo anaenda kuwa Kamanda wa Polisi Kikosi cha Tazara

IGP Sirro amewataka Makamanda wa Polisi wa mikoa nchini, kuendelea kuwajibika ipasavyo katika kuhakikisha ajali hazitokei katika maeneo yao


Rais Magufuli ataja sababu za kumtumbua Mwigulu Nchemba
https://www.youtube.com/watch?v=Piazp5R_qBg&t=5s

No comments:

Powered by Blogger.