Header Ads

Unachotakiwa kufanya ikitokea Condom imepasuka wakati wa tendo

Karibu uhondo TV sehemu pekee utapata habari za siasa, michezo, burudani na stlye za maisha.
Moja ya kitu leo tunakileta kwako ni hatua nne utakazotakiwa kufuata endapo kondomu itapasuka wakati wa tendo la ndoa.
Hatua ya kwanza unatakiwa Kuwa mtulivu na baadaye tafuta kondomu hiyo iliopasuka. Mara nyengine vipande vya mpira huo wa kondomu unaweza kuingia ndani ya mwili. ingiza vidole vyako ndani yake ishike na kuitoa nje.
Mipira ama vipande vya kondomu vinavyosalia ndani ya mwili wa binadamu vinaweza kusababisha hasira hivyo basi ni muhimu kuangalia na kuhakikisha kuwa umetoa kondomu yote.

Hatua ya pili unaambiwa Tumia dawa za kuzuia kushika mimba iwapo hamjakubaliana kupata mtoto pamoja, Dawa hizi zinapaswa kutumiwa katika kipindi cha saa 72. Zinauzwa dukani-ikimaanisha kwamba zinapatikana katika maduka ya dawa. Iwapo huna mpango mbadala unaweza kutumia dawa za kupanga uzazi.

Hatua ya tatu una shauriwa Kupimwa magonjwa ya zinaa hususan HIV iwapo hujui hali ya mwenzako Nenda katika kituo cha dharura karibu nawe na umwambie daktari yaliofanyika.
Aidha unaweza kuchukua dawa aina ya Post Exposure Prophylaxis (PEP) katika kipindi cha saa 72.
PEP ni mchanganyiko wa dawa za kukabiliana dhidi ya virusi vya ukimwi ambazo zinakuzuiwa kutoambukizwa HIV iwapo mwenzako ni mwathiriwa.
Kumbuka kwamba kila ugonjwa wa zinaa una muda wake wakati unapoambukizwa na wakati utakapoonyesha unapopimwa. Unashauriwa kufanyiwa vipimo zaidi vya vya magonjwa ya zinaa baada ya mwezi na baada ya miezi sita ili kujua hali yako.

Hatua nyingine unayoshauriwa ni kuChunguza kilichotokea
Wapenzi wengi huruka hatua hii-hayo ni makosa makubwa, kwa sababu ni hadi utakapoelewa ni kwa nini mpira huo ulipasuka ndiposa unaweza kujiweka katika hatari nyengine. Hivyobasi jiulize swali hilo.

Je mpira huo wa kondomu ulipasuka kwa sababu wakati wake ulikuwa umekwisha?
Iwapo hilo ni kweli unaweza kutupa paketi ulio nayo na kununua pakiti nyengine . Ziweke mbali na joto ama hata mwangaza na usizibebe katika kipochi chako na usizifungue kwa kutumia makasi ama meno.

-Je mpira huo wa kondomu ulipasuka kwa sababu ulivaliwa vibaya?
Weka mafuta ndani ya kondomu hiyo iwapo utahitaji , lakini hakikisha kuwa hutumii mafuta nje ya mpira huo, Finya eneo la mbele la mpira huo ili kutoa upepo Ukishavaa kondomu hiyo wacha nafasi mbele ya mpira huo ambayo itaweka shahawa.

-Je mpira huo wa kondomu ulipasuka kwa kuwa ulikuwa mdogo sana?
Pima ukubwa wa uume wake wakati unaposimama. Halafu uangalie chapisho hili ili kujua ni ukubwa gani wa kondomu unaopaswa kutumia. Unaweza kushangaa!

-Je mnpira huo wa kondomu ulipasuka baada ya kuupaka mafuta?
Utumizi wa mafuta kama vile ya Olive ama mafuta ya nazi unaweza kuwa hatari kwasababu yanaweza kufanya kondomu kupasuka

Kumbuka kwamba ajali za kondomu zinaweza kumtokea mtu yeyote.
Basi kwa habari za siasasa , michezo, burudani na style za maisha subscribe youtube channel yetu ili uzipate kwa haraka kila tutakapokuwa tunaweka

No comments:

Powered by Blogger.