Header Ads

ALIYESIMAMISHWA NA MWIGULU ARUDI KAZINI

Miongoni mwa habari kubwa mitandaoni ni pamoja na Picha inayosambaa ikimuonesha Mkurugenzi wa Idara ya Usajili wa Vyama vya Kijamii katika Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi Marlin Komba ambaye alisimamishwa kazi Juni 8, 2018 na Aliyekuwa Waziri wa Wizara hiyo Mwigulu Nchemba kutokana na barua iliyosambaa mtandaoni ikiwa na sahihi yake. Barua hiyo ililitaka kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) kufuta waraka wake Pasaka.

Picha hii inayomuonesha Marlin Komba akisalimiana na Waziri mpya wa Wizara hiyo Kangi Lugola imetoa tafsiri kwa watu wengi kwamba Marlin Komba amerudi kazini .


Kwa mastori makali kama haya endelea kukaa karibu na chaneli yetu ya UHONDO TV pamoja na Uhondo Habari kwenye mitandao ya kijamii.


No comments:

Powered by Blogger.