Header Ads

NOMA SANA: Raia wa kigeni akitaka kuoa analipa kodi




Miongoni mwa mastori makali ya kukusogezea leo ni pamoja na hii ya kutoa kwa Mfalme Mswati wa swaziland ametuma mswaada bungeni akitaka kutungwa kwa sheria mpya kwa raia kutoka nje ya nchi hiyo kulipa kodi watakapofunga ndoa na wanawake nchini Swaziland kwa kutozwa kiasi cha dola 2,200.

Unaambiwa kwamba Mfalme Mswati ametuma mswaada huo bungeni huku akidai kuwa sheria hiyo ni kwa ajili ya kuwalinda wanawake nchini humo.

“ Lengo la sheria hii ni kuwalinda wanawake na matendo ya unyanyasaji kutoka kwa wapenzi wao wa kigeni wanaotumia njia ya kuoa wanawake wetu kwa ajili ya kupata uraia hayo yamenukuliwa kutoka kwa Msemaji wa Serikali Percy Simelane.

Aidha mswada huo umepingwa vikali na mmoja wa wanaharakati wa kutetea haki za wanawake Dumsane Dlamini akidai kuwa sheria hiyo itawanyima haki wanawawake nchini Swaziland maana wanawake hao huwapenda wanaume wa kigeni kwa utanashati na wanajua thamani ya mapenzi.

Lakini ikumbukwe mnamo mwaka  2016, Wizara ya mambo ya Kigeni ilianzisha mpango wa kutoa uraia kwa wageni nusu milioni hasa kutoka Asia ambao watakuwa sehemu ya idadi ya raia 1.3 milioni ya wananchi wote wa Swaziland.

Kwa mastori makali kama haya endelea kukaa karibu na Uhondo Habari ndani ya saa 24 

No comments:

Powered by Blogger.